Head image
Govt. Logo

Hits 110025 |  2 online

           


Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais amezishauri taasisi za Serikali na binafsi zinazotoa huduma kwa jamii kutoa kipaumbele kwa Watu wenye mazingira maalum
news phpto

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe Dkt Saada Mkuya Salum amezishauri taasisi za Serikali na binafsi zinazotoa huduma kwa jamii kutoa kipaumbele kwa Watu wenye mazingira maalum wakiwemo Watu wenye Ulemavu wa Uziwi

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe Dkt Saada Mkuya Salum amezishauri taasisi za Serikali na binafsi zinazotoa huduma kwa jamii kutoa kipaumbele kwa Watu wenye mazingira maalum wakiwemo Watu wenye Ulemavu wa Uziwi

Dkt Saada ameyasema hayo wakati akiyafungua mafunzo maalum ya lugha ya alama kwa watendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ZSSF yaliyoaandaliwa na Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu katika ukumbi wa ZSSF Kariakoo

Ameipongeza ZSSF kwa kuwa mfano bora kwa mashirika ya serikali kuonesha kwa vitendo na dhamira njema ya kuwahudumia wananchi wa makundi yote kwa kuanza na lugha ya alama ambayo itawasaidia viziwi kupata huduma wanazozitoa kwa uhakika bila ya gharama ya kutafuta mkalimali

Aidha Dkt Saada ameiomba ZSSF wasiishie hapo bali kutafuta na njia nyengine ya kuwasaidia Watu wenye Ulemavu wa Uoni kwa kuangalia uwezekano wa kutengeneza kadi za ZSSF zenye alama ya nukta nundu

“Naziomba na taasisi za Serikali ili tuwe na jamii shirikishi basi sasa hata vitabu vya sera na sheria na vyenginevyo tuhakikishe tunaandika kwa nukta nundu ili wenzetu wenye Ulemavu wa Uoni nao waweze kusoma maendeleo ya nchi yetu mfano nzuri tulivyoanza Ofisi ya Mkamu wa Kwanza wa Rais Bajeti ya Serikali tuliwazingatia kwa kutoa vitabu vilivyoandikwa kwa kutumia nukta nundu”

Kufanya hivyo kutahusisha huduma wanazozitoa kuwa bora zaidi na zinazokwenda na wakati huu wa ukuwaji wa teknologia pamoja na kuziomba taasisi nyengine kujipanga ili ziweze kutoa huduma kwa ufanisi bila ya kuwaacha wengine kama Watu wenye Ulemavu

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kupitia Baraza la Watu wenye Ulemavu linatambua kuwa fursa mpya ya uchumi wa buluu ni kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wote wa Zanzibar hivyo imejipanga kuandaa mpango mkakati wa kuona lugha ya alama inapewa kipaumbele kufundishwa kwenye taasisi zote zinazotoa huduma kwa jamii

Nae Mkurugenzi wa Baraza la Watu wenye Ulemavu Mhandisi Ussy Khamis Debe amesema mafunzo ya lugha ya alama yameanzishwa baada ya kuonekana kuna upungufu kwa taarifa kwa Watu wenye Ulemavu wa Uziwi

Mhandisi Ussy amesema kati ya changamoto wanazozipata Watu wenye Ulemavu wa uziwi kutopata taarifa sahihi kwa wakati muafaka na ndio maana Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu likaamua kuendelea kutoa elimu hii ya lugha ya alama kwa taasisi tofauti

Mafunzo kama hayo pia hutolewa na Jumuiya ya wakalimani wa lugha ya alama JUWALAZA, Chama cha Viziwi Zanzibar CHAVIZA na chuo cha SUZA, hii ni awamu ya pili ya muendelezo wa mafunzo ya lugha ya alama kwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar.

Huduma za Tehama

Barua Pepe

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

ZEMA ZAC DDA IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 2808, Migombani, Zanzibar
Tel.: +255(24)2232474 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2232475 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2232476
Email: info@omkr.go.tz