Head image
Govt. Logo

Hits 110221 |  3 online

           


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais amewataka watendaji wa ofisi hiyo kujitathmini na kujipanga upya katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi
news phpto

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mh Harusi Said Suleiman amewataka watendaji wa ofisi hiyo kujitathmini na kujipanga upya katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi ili lengo la serikali la utoaji wa huduma bora kwa wananchi liweze kufikiwa kwa wakati

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mh Harusi Said Suleiman amewataka

watendaji wa ofisi hiyo kujitathmini na kujipanga upya katika utekelezaji wa majukumu yao ya

kazi ili lengo la serikali la utoaji wa huduma bora kwa wananchi liweze kufikiwa kwa wakati.

Mh. Harusi ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na watendaji wa Idara, Tume na Mamlaka

zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais katika mkutano wa kujitambulisha kufuatia

uteuzi wake hivin karibuni ili kuona maendeleo ya taasisi hizo kwenye ukumbi wa mkutano

Gombani Chake Chake.

Amesema ni wajibu wake watendaji na wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii na kufuata

muongozo wa utumishi ambapo pamoja na kujitathmini kiutendaji, kuona kipi ambacho

amekifanikisha kwa muda wa wiki nzima ambacho kimeweza kuleta tija kwa taasisi na

wananchi.

Aidha Mh. Harusi amewaambia watendaji hao kuzidisha ari na nguvu ya kiutendaji kwa

wananchi wanaohitaji huduma na kutatua changamoto zao ukizingatia kuwa sekta za ofisi hii ni

mtambuka hivyo hawapaswi kukaa ofisini bali wajitoe kufikisha elimu na huduma stahiki kwa

wanajamii.

“watendaji hakikisheni mnashirikiana pamoja ili wale wanaokufateni mnaowangoza nao waone

kuwa viongozi wao wapo makini na hakutakuwa na mwanya wa kufanya yaliyo sio bali kama

zipo changamoto zigeuke kuwa fursa kwa kuwa wabunifu wa mipango mipya yenye kuleta tija

“alisisitiza Bi Harusi

Mapema Mhe Harusi alionana na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mh. Mattar Zahor Masoud

na kufanya mazungumzao mafupi ofisini kwake ambapo viongozi hao wote wameahidi

kushirikiana pamoja ili kufanikisha majukumu yatayoleta mafanikio ndani ya mkoa huo kwa vile

masuala yanaosimamiwa na ofisi hio yanamgusa kila mtu.

Afisa Mdhamini wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Bw Ahmeid Abubakar amemuahidi

Waziri Bi Harusi kwa kushirikiana na watendaji wanahakikisha wanatekeleza majukumu yao

vyema kusimamia miradi ya maendeleo na kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi

Mh.Harusi amezitembelea Idara na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira, Mamlaka ya Kudhibiti

na Kupambana na Dawa za Kulevya, Baraza la Watu wenye Ulemavu na Tume ya UKIMWI pia

ameikaguwa miradi ya maendeleo ukiwemo Mradi wa ujenzi wa tuta la kuzuwia maji ya chumvi

yasiingie katika mashamba uliopo Tovini

Kwengine ni kuona mradi wa ujenzi wa Ukuta wa mawe katika fukwe ya mwambao wa eneo la

Msuka, mradi wa ujenzi wa mabwawa ya maji machafu ulipo Kichungwani, pamoja na kufika

Likoni Kojani kuangalia eneo linalotarajiwa kujengwa ukuta wa kuzuwia mmongonyoko wa

fukwe ambao pia utaunusuru mbuyu wa asili uliopo eneo hilo ambao kwa sasa upo hatarini

kuanguka

Huduma za Tehama

Barua Pepe

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

ZEMA ZAC DDA IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 2808, Migombani, Zanzibar
Tel.: +255(24)2232474 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2232475 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2232476
Email: info@omkr.go.tz