Head image
Govt. Logo

Hits 110421 |  6 online

           


SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) imepitisha sheria ya watu wenye ulemavu pamoja na kuunda mabaraza ya wilaya.
news phpto

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) imepitisha sheria ya watu wenye ulemavu pamoja na kuunda mabaraza ya wilaya kwa lengo la kuhakikisha wanapata haki zao kama wanavyopata watu wengine.

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) imepitisha sheria ya watu wenye ulemavu pamoja na

kuunda mabaraza ya wilaya kwa lengo la kuhakikisha wanapata haki zao kama wanavyopata

watu wengine.

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Harusi Said Suleiman ameyasema hayo

mara baada ya kumaliza kwa ziara yake katika Mkoa wa Kaskazini Unguja. Amesema sheria

hiyo imeshakamilika na ipo tayari kutumika ambayo itapita katika sekta zote na kusaidia kutatua

changamoto ambazo zinawakabili watu wenye ulemavu pamoja na kupatiwa haki na fursa zote.

“Sheria ya watu wenye ulemavu tayari imeshapitishwa na itakuja katika sekta zote, pamoja na

kuanzishwa kwa mabaraza ya Wilaya, ombi langu kwenu naomba tushirikiane kwa pamoja

katika kusaidia kutatua changamoto wanazozipata pamoja na kuwapatia fursa muhimu kwao”.

Waziri Harusi ametoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kuwaficha watoto wenye ulemavu ambapo

amesema kufanya hivyo ni kuwanyima haki zao za msingi pamoja na kuwadhalilisha. Aidha

Waziri huyo amesema ofisi yake ipo katika mpango wa kuhakikisha wananchi wanarudisha hali

ya mazingira ya kijani katika visiwa vya Unguja na Pemba.

Amesema wameamua kufanya hivyo kutokana na kuona kijani inapotea katika visiwa hivi

ambapo bila ya kufanya hivyo madhara mengi yanaweza kupatikana. “Tusipoweka mpango

maalum wa kuirudisha kijani katika nchi yetu madhara na matatizo mengi yanaweza kutufikia,

tukifanya hivyo tunaweza kujijenga na kuimarisha ardhi pamoja na kuepukana na majanga ya

aina mdali mbali”.

Hivyo, Waziri Harusi amewataka wamiliki wa hoteli mbali mbali visiwani humu kuiga mfano

wa hoteli ya Zuri ambayo imejikita katika kulinda na kuhifadhi mazingira. Amesema wananchi

waridhie kutunza mazingira na kutunza miti na kuhakikisha haiba ya mji inaonekana.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Ayoub Mohammed Mahmoud amesema katika Mkoa

wake tatizo la dawa za kulevya limepungua kwa kiasi kikubwa. Amesema wanachokifanya hivi

sasa ni kufuatilia kwa karibu katika hoteli na nyumba za kulala wageni kwa lengo la kuhakikisha

usambazaji na uuzwaji wa biashara hiyo haramu unaondoka katika Mkoa huo. “Serikali ya Mkoa

inawashukuru sana masheha kwa juhudi wanazozichukua katika kuhakikisha inavunja magenge

ambayo yanasabisha kuwepo kwa biashara hiyo, lakini tumeanzisha ulinzi shirikishi katika

kuondoa hilo tatizo”.

Nae muelimishaji rika kituo cha huduma rafiki Nungwi, Khamis Ali Makame amesema

kuanzishwa kwa kituo hicho kimesaidia vijana wa eneo hilo na maeneo mengine kwenda

kujifunza maswala mbali mbali. Ameeleza kwamba kuwepo kwa kituo hicho cha huduma rafiki

vijana wengi wamefanikiwa kupata elimu ambayo inawasaidia kujitambua katika maisha yao ya

kila siku. Amefahamisha kwamba vijana wengi wanaofika katika kituo hicho ni wanafunzi wa

skuli na vijana wa mitaani ambapo kwa siku wanafika zaid ya 30 katika kupata elimu ya mambo

mbali mbali.

Katika ziara hiyo Waziri Harusi alitembelea maeneo mbali mbali ikiwemo kituo cha huduma

rafiki, soko na maeneo mazingira ya bahari Nungwi, kikundi cha watu wenye ulemavu

Fukuchani na hoteli ya Zuri iliyopo Kendwa.

Huduma za Tehama

Barua Pepe

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

ZEMA ZAC DDA IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 2808, Migombani, Zanzibar
Tel.: +255(24)2232474 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2232475 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2232476
Email: info@omkr.go.tz