Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php70/sess_68ce208c5781bf5c52bb28519b922503, O_RDWR) failed: No space left on device (28) in /home/omkr/public_html/sess.php on line 17

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php70) in /home/omkr/public_html/sess.php on line 17
fullview :: First Vice President office, Zanzibar
Head image
Govt. Logo

Hits 4947 |  1 online

           


TULINDE MAZINGIRA NA TUACHANE NA UHARIBIFU
news phpto

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,Mheshimiwa Harusi Said Suleiman akiwa katika ziara ya kimazingira na kukagua Maeneo yaliyoathiriwa na uchimbaji wa Mashimo Hatarishi ya chini kwa chini (Tunnel) Pembezoni mwa ukanda wa Bahari katika Kijiji cha Mtende,Mkoa wa Kusini Unguja:tarehe 21.02.2024.

Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa kwanza wa Rais, Mhe. Harusi Said Suleiman amewataka Wananchi na Wawekezaji kulinda Mazingira ili uwekezaji wao uwe endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Mhe. Harusi ameyasema hayo wakati wa ziara ya kukagua miradi mbali mbali ya Uwekezaji na kuona jinsi inavyohifadhi mazingira.

Amesema, utunzaji wa mazingira ni muhimu na kuahidi kuwa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais itaendelea kutoa elimu na hamasa ya utunzaji wa Mazingira ili Wananchi na Wageni waweze kujua umuhimu wa Mazingira Nchini.

Aidha, amemtaka Mmiliki wa mradi wa Ujenzi wa Hoteli ya Umbe Villas beach and Bangalore kusimamisha uchimbaji wa shimo kwa ajili ya kutengeneza njia ya ufukweni ili kujikinga na matatizo yanayoweza kujitokeza.

‘‘Huu ni uvunjifu wa Sheria na unaweza kuleta athari za kimazingira kwa jamii hivyo naomba Shimo hili lifukie mara moja.’’ Alisisitiza Waziri Harusi.

Huduma za Tehama

Barua Pepe

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

ZEMA ZAC DDA IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 2808, Migombani, Zanzibar
Tel.: +255(24)2232474 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2232475 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2232476
Email: info@omkr.go.tz