Head image
Govt. Logo

Hits 111801 |  2 online

           


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais amefanya ziara ya kutembelea Kambi ya Waanika madagaa iliyopo Mangapwani na
news phpto

Mhe Dkt Saada Salum Mkuya amefanya ziara ya kutembelea Kambi ya Waanika madagaa iliyopo Mangapwani na kushuhudia mazingira yasiyoridhisha kutokana na kukosekana kwa miundo mbinu muhimu katika kambi hio

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe Dkt Saada Salum Mkuya amefanya ziara ya kutembelea Kambi ya Waanika madagaa iliyopo Mangapwani na kushuhudia mazingira yasiyoridhisha kutokana na kukosekana kwa miundo mbinu muhimu katika kambi hio

Dkt Saada ameahidi kukaa pamoja na wahusika wengine pamoja na kamati ya waanika madagaa ili kuondosha changamoto ya eneo hilo lenye harakati za kiuchumi zinazopelekea kuingia na kutoka kwa wenyeji na wageni

Hatua hizo ni pamoja na kupeleka wataalaamu kutoka Mazingira Tume ya UKIMWI na Tume ya Kitaifa Kuratibu na kupambana na Dawa za Kulevya ili kutoa elimu kwa usalama wa waanika madagaa na wauzaji wa jumla kwenye kambi hiyo

Dkt Saada amesema hatua nyengine ni pamoja na kuchukuliwa hatua za haraka kwa kuweka miundo mbinu ya uhakika ili kuepuka maradhi yanayoweza kutokea ikiwemo ya mripuko kama kipindupindu

Nao baadhi ya wanakambi wa eneo hilo wamelalamikia kutofanyiwa kazi malalamiko yao ya muda mrefu ikiwemo kupatiwa huduma ya maji na vyoo ambapo wameshauri fedha zinazochangishwa na Halmashauri kila mwezi kuwasaidia kuweka miundombinu ya kudumu

Katika ziara hio Dkt Saada amefuatana na Mwakilishi wa Jimbo la Bumbwini Mhe Mtumwa Peya na kukiri changamoto hio ni ya muda mrefu na tayari wameshakaa pamoja na Kamati ya waanika madagaa kwa kushirikiana na sheha wa shehia na taarifa ya changamoto hizo zimeshafikishwa kwa Mkuu wa Wilaya Kaskazini B

Zaidi ya watu 400 ya waaanika madagaa hueka kambi kwa wakati mmoja wakati wa bamvua la msimu wa madagaa ambapo wanunuzi wakubwa ni Wacongo ambao nao wamelalamikiwa bei ndogo wanayonunulia ikilinganishwa na gharama kubwa wanazotumia waanika madagaa hao

Aidha wauza madagaa hao wameiomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuweka viwango maalum kwa wanunuzi wa madagaa kama inavyowekwa bei za mchele ili kumkomboa Mwananchi kiuchumi

Huduma za Tehama

Barua Pepe

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

ZEMA ZAC DDA IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 2808, Migombani, Zanzibar
Tel.: +255(24)2232474 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2232475 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2232476
Email: info@omkr.go.tz